Friday 10 April 2015

UKIWA NA VITU HIVI VITATU UTAKUWA NA MAISHA BORA


Maisha ni jinsi unavyoyachukulia mwenyewe. Maisha bora unayaandaa mwenyewe. Kuwa na maisha bora na ya furaha kuna vitu ambavyo unatakiwa kuwa navyo. Vitu hivyo huwezi kuletewa na mtu yeyote isipokuwa wewe mwenyewe. Huhitaji pesa, umaarufu ama madaraka ili uwe na maisha bora na furaha. Simaanishi kwamba pesa, madaraka au umaarufu havihitajiki maishani la hasha, namaanisha kuwa kuwa navyo bila kufanya haya ni ngumu kuwa na maisha bora.
Kubadili vitu unavyoweza kubadili
Kubali usikubali kuna vitu ambavyo unaweza kuvifanya ama kuvibadili maishani, hivi vibadili haraka iwezekanavyo. Usisubiri aje mtu mwingine avibadili kwani mara nyingi vyote vipo ndani uwezo wako. Kubadili tabia zako hakuhitaji usaidizi wa profesa wako wa chuo, bosi wako wala mwenyekiti wako wa mtaa. Je huwezi kubadili tabia yako ya uvivu? Huwezi kubadili tabia yako ya ufujaji wa pesa? Huwezi kuamua kuwa na mafanikio? Huwezi kuwa mwekezaji? Bila shaka tabia hizo na nyinginezo nyingi ziko ndani ya uwezo wako na ukiamua kubadili hakika