Showing posts with label Uchumi & Biashara. Show all posts
Showing posts with label Uchumi & Biashara. Show all posts

Monday, 4 July 2016

Choma meli yako sasa

Ndugu msomaji napenda kutumia wasaa huu kuweza kukusalimia kabla sijaanza kukushirikisha niliyonayo leo. Nianze kwa kukusimulia hadithi moja:

Hapo zamani kuna kiongozi wa nchi fulani alienda vitani na jeshi lake katika nchi ya kigeni kwa kutumia usafiri wa meli. Alipofika pwani ya nchi ya adui aliamuru jeshi lake kuchoma meli waliyokwenda nayo. Aliwaambia wapiganaji wake kwamba kwa sasa wana machaguo mawili tu ambayo ni kushinda ile vita na ni lazima washinde ama kufa wote kwani hawawezi kutoka salama huko kwa kutoroka kwani wameshachoma moto meli yao. Wasiposhinda maana yake watauawa ama watakuwa mateka ama washinde vita na warudi nchini kwao salama. Hapo sasa kukawa hakuna jinsi zaidi ya jeshi lake kuwa na dhamira moja tu ya kushinda

Thursday, 12 March 2015

Makosa 10 ya kuepuka ili upate mafanikio ya kipesa


Pesa ni chombo kinachotumika kupima thamani ya vitu kama huduma na bidhaa. Pesa hutumika kubadilisha bidhaa na huduma mbalimbali. Kupata na kuhifadhi pesa imekuwa ni changamoto kubwa sana. Hivyo basi ili uweze kufanikiwa yakupasa kujifunza kuhusu pesa. Watu wengi waliofanikiwa wamejifunza na kuelewa pesa.
  1.  Matumizi yasizidi mapato
Ili uweze kufanikiwa kimaisha hasa katika suala la pesa, basi yakupasa kutumia pesa chini ya kiwango unachoingiza. Hii itakusaidia kuweka akiba kwa matumizi ya baadae na

Wednesday, 3 December 2014

Madhara ya kuwa mdaiwa sugu



Katika maisha huwezi kupata kila kitu unachokitaka, pia huwezi kuhitaji kila unachokipata. Hakuna mtu yeyote duniani ambaye amejitosheleza kwa kila kitu na asihitaji msaada wa mtu mwingine yeyote, hata Billgates huhitaji msaada wa watu wengine ili aweze kuishi na kustawi katika maisha na biashara zake. Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kuishi maisha yake yote ya hapa duniani bila kukopa,hivyo basi kukopa sio jambo baya wala la ajabu. Jambo lililo baya ni kuwa mdaiwa sugu ama kutolipa madeni. Watu wengine hushindwa kulipa madeni si kwa sababu hawana uwezo wa kuyalipa bali hawaoni umuhimu ama hujisahau katika hilo.
Lengo la makala hii fupi ni