Uongozi
ni kuonyesha njia kwa wengine. Uongozi thabiti huweza kushinda nyakati ngumu
katika hii dunia, huku uongozi mbovu ukiitumbukiza jamii katika majanga na
majuto. Dunia hii ishawahi kuwa na viongozi bora sana. Je unamkumbuka Abraham
Lincoln, Mwl J.K. Nyerere, Sokoine, Mandela na wengi wengineo ambao wamekuwa
mfano wa kuigwa vizazi kwa vizazi. Najua kuna wabovu pia ambao unawafahamu
kuanzia ulimwengu wa kwanza mpaka wa tatu. Hayati Dr. Myles Munroe aliwahi
kusema ‘jeshi la
kondoo linaloongozwa na simba ni rahisi kulishinda kundi la simba linaloongozwa
na kondoo’. Maana yake
Hakuna Adui Mkubwa Kama Muda Unaoupoteza Mwenyewe…
-
…Rafiki yangu,Wengi wanadhani tatizo lao ni bahati mbaya.Wanashangaa
kwanini wengine wanapata kila kitu kwa urahisi,wakidhani wao
wamekataliwa.Lakin...