Thursday 19 March 2015

Namna ya kuwa rafiki bora


Katika makala iliyopita tuliona jinsi marafiki walivyo muhimu katika maisha yetu. Hivyo basi leo nimeona ni bora nijaribu kueleza namna ya kuwa rafiki bora. Ili kuwa rafiki bora huna budi;

Image result for pictures of friends
   1. Jifunze kusamehe
Kama ilivyo kwa penseli kuwa na ufuto ndivyo na marafiki walivyo. Katika dunia hii hakuna mtu yeyote aliye mkamilifu. Kama ni hivyo basi kila mtu hutenda makosa na kama kama anakosea basi yapasa kusamehewa ili maisha yasonge mbele. Hupaswi kuwa na kinyongo. Samehe na sahau kabisa kwani msamaha bila kusahau ni sawa na kulima shamba bila kupalilia. Kama ilivyo safari ambayo hupitia milima na mabonde mingi ndivyo ulivo urafiki. Kadiri mtakavyokaa pamoja na kusameheana mengi ndivyo na urafiki wenu utakavyostawi.
 2. Kuwa msikilizaji mzuri
Kila mtu anahitaji kusiilizwa. Kama ambavyo wewe ungependa kusikilizwa ndivyo na rafiki yako anavyotaka asikilizwe na wewe. Ili kujenga urafiki imara basi jiandae kusikilza marafiki zako na inapobidi kuwasaidia.
 3. Wekeza katika urafiki wenu
Kama shamba linavyohitaji matunzo ndivyo na urafiki unavyohitaji malezi. Unapaswa kutafuta kitu ambacho mnapenda kukifanya kwa pamoja hata kama utakuwa umetingwa sana na kazi ama una msongo angalau mara moja kwa wiki.  Mfano mnaweza kukaa sehemu tulivu na kubadilishana mawazo, kutembelea mbuga za wanyama, kucheza/kuangalia pamoja mchezo mnaoupenda na hata kutembeleana na mengine mengi.
 4. Kuwa kama rafiki unayemtaka
Mtendee rafiki yako kadiri wewe unavyotaka kutendewa. Maana yake mtendee rafiki yako mambo mema, mambo ambayo hata wewe ungependa kutendewa. Kumbuka hakuna mtu anayependa kutendewa mambo mabaya.
 5. Usimbane sana rafiki yako.
Usimbane sana rafiki yako kwamba muda wote muwe pamoja bali mpe nafasi aamue mwenyewe. Atahitaji kuwa na watu wengine tofauti na wewe. Pia usiwe tegemezi sana kwake kwani utahatarisha urafiki wenu. Pia usiweke masharti magumu katika urafiki wenu bali acha urafiki wenu ukue katika ya hali yake ya asili kwani ukiulazimisha utakufa siku moja.
Asante na karibu kwa maoni, ushauri na nyongeza

0 comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.